SIKILIZA BONGO FLAVA MPYA HAPA


fetty
Quantcast

OUR CHART


NGOMA GANI KALI YA MWEZI

JIUNGE NAMI KWENYE UPANDE WA EMAIL AU SIO


fetty
Quantcast

Monday, December 7, 2009

NGOMA MPYA ZILIZOTUFIKIA BLOGUNI


moja kati ya ngoma mpya nilizozikamata wiki hii ni pamoja na ngoma ya K-lyn inayoitwa Not a flurt, imefanyika ndani ya studio za b-hits producer akiwa ni Pancho latino

Sunday, December 6, 2009

UJUMBE WA IDDY TENDEGA MDAU KWA WATANZANIA


Mtanzania mwenzangu,

Kwa mtazamo wa kawaida na wa kijuujuu,watanzania tunajulikana kwa kuwa
wazalendo sana. Tunasemekana kuwa watu tunaoipenda nchi yetu na
tunaojipenda pia. Tumejipa majina kemkem katika kujivunia utanzania
wetu. Nchi yetu inajulikana miongoni mwa wengi kama “bongo” yaani
akili.

Zamani zile “bongo” ilikuwa ni jiji la Dar-es-salaam tu,siku hizi
bongo ni Tanzania nzima au niseme Tanganyika nzima ingawa najua kuna
watu wanajidai kwamba jina Tanganyika halimo katika msamiati wao. Huko
ni kujidanganya na kupotosha historia.

Kwa wengi, ingawa sera za kiuchumi za Mwalimu Nyerere zilifeli,sera za
kijamii zilifanikiwa sana. Mojawapo ya mafanikio ya kijamii ni pamoja
na hili la “uzalendo”.Mapenzi yasiyo kifani kwa nchi yetu,popote
tulipo tunaiota Tanzania nk.

Leo nataka niangalie kidogo kama kuna ukweli wowote kwamba tunaipenda
sana nchi yetu. Lakini kabla sijaenda mbele sana naomba niweke wazi
kwamba mimi siamini kama tunaipenda kweli nchi yetu kama tunavyodai.
Naona tunashabikia nchi yetu lakini hatuipendi nchi yetu.

Kwani nchi ni nini basi? Nchi ni mbuga za wanyama? Nchi ni maeneo ya
kijografia aliyotuwekea mkoloni? Nchi ni mashamba yasiyozalisha?
Tafsiri ya nchi inaweza kuwa ngumu sana, kila mtu anaweza akawa na
tafsiri yake na kila mmoja akawa sawa.Kwangu mimi nchi ni yote hayo
hapo juu na mengineyo pamoja na watu wake. Sipati picha na “nchi” bila
watu.

Nchi yetu ipo ilipo kwa sababu ya ukosefu wa “uzalendo”.Tofauti na
madai ya wengi wetu,mapenzi (uzalendo) kwa nchi yetu ni kama hakuna.
Kama unaipenda nchi yako,utaiibia? Kama unaipenda nchi yako utakula
rushwa? Kama unaipenda nchi yako hutoonyesha wazi bali mpaka utolewe
kashfa ndio uzinduke? Kama unaipenda nchi yako utakwepa kodi? Kama
unaipenda nchi yako utakuwa mzembe kazini? Kama unaipenda nchi yako
utaloga wenzako?

Kama unaipenda nchi yako utaacha kuichagulia viongozi bora na sio kwa
kusubiri upewe rushwa? Kama unaipenda nchi yako utaikana? Kama
unaipenda nchi yako utaachia wageni waje na kuchuma uchumi wote wa
nchi ilhali wewe umekaa tu kibarazani?

Kama unaipenda nchi yako utakuwa huijui hata historia yake achilia
mbali jiografia yake? Kama unaipenda nchi yako utajifanya huijui hata
lugha rasmi ya nchi yako ili mradi uonekane bora miongoni wa kundi
fulani la watu? Kama unaipenda nchi yako mbona huungi mkono chochote
cha kitanzania kiwe ni sanaa au bidhaa za nyumbani?

Maswali yanayohoji “uzalendo” wetu ni mengi kupita kiasi. Ninaposema
hatuipendi nchi yetu huwa najaribu kuangalia jinsi gani wengi wetu
tunaishi katika “uzalendo” kwa kufanya hasi ya mambo niliyoyataja hapo
juu ambayo ni machache tu. Je “uzalendo” wetu ni ushabiki tu usio na
maana yoyote? Tunaposema tunaipenda nchi yetu huwa tunamaanisha nini?

Nyerere aliturithisha rushwa? Nyerere aliturithisha uzembe na uvivu,
kutowajibika? Hiyo ndio misingi ya taifa letu? Ni wazi kabisa kwamba
Hayati Mwalimu Nyerere alijitahidi sana kuhakikisha kwamba uzalendo
kwa nchi yetu unakwenda na vitendo. Kama alifanikiwa au alifeli pia
jibu lipo miongoni mwetu sisi wenyewe,kila mmoja wetu. Tafakari.

Nimefikia kuandika juu ya “uzalendo” tena kwa sababu naamini huo ndio
msingi wa kujenga nchi. Hizi nchi za wenzetu zimejengwa kwa kutumia
msingi wa uzalendo. Ukiwa hapa Canada au Marekani unaona kabisa jinsi
gani wenzetu wanazipenda nchi zao.Utathibitisha hilo kwa kuangalia
jinsi ambavyo wanajitolea pindi wanapohitajika.

Wanaamini kwamba nchi ni yao na wao ndio wa kuijenga au
kuibomoa,chaguo ni lao. Kwa bahati mbaya kwetu sisi tunadhani kuwa
“mzalendo” ni pale tu unapotamka kwamba unaipenda nchi yako huku
vitendo vyako vikithibitisha chuki mbaya uliyonayo.

Najua wengi mtasema “ah iddy,sisi tunaipenda nchi yetu sana tu,tatizo
ni viongozi wetu ndio wanatuangusha” Nitakuuliza,unadhani hizi nchi
zilizoendelea huwa zinaongozwa na malaika? Jibu ni hapana,zinaongozwa
na watu,tena wengi wao ni wala rushwa kama wetu tu, tofauti ni kwamba
wananchi wanatambua kwamba uzalendo ni pamoja na kuhakikisha
tunachagua viongozi na sio watawala.

Na isitoshe wanaamini kwamba kiongozi akikosea basi hana budi
kuondolewa.Hakuna kulindana kwa sababu kama unamlinda kiongozi
mbovu,basi hata wewe huna mapenzi kwa nchi yako. Nchi ni watu na sio
viongozi peke yao.

Kwa kumalizia naomba ndugu msomaji,baada ya kumaliza kusoma hii
makala,jiulize nini unaifanyia nchi yako ili kuthibitisha “uzalendo”
wako? Tuipende nchi yetu kwa vitendo na sio maneno.
contact me via email:iddy20@yahoo.com nikiwa tz natumia 0719283959

Friday, December 4, 2009

MDAU WA KARIBU SANA BLOGUNI


MILTON KEYNES STAND UP...


INFINITY ENT'S pres,CHRISTMAS EVE Party 24th DECEMBER 09 at SPICE LOUNGE,3 savoy crecent, Theatre District,MILTON KEYNES.mk9 3pu,DJ HABIBU & DJ DOUBLE T will make it happen.BONGO FLAVAS,R&B,RAGGA,OLD SKOOL. 10Pm till Late,Admission:£10 B4 12:VIP TICKETS AVAILABLE AT THE DOOR....HABARI NDIO HIYO.....

Nitashukuru sana kwa msaada wako

Mdau wako UK

N.B Naomba email yangu usiiweke Tafadhali..

Wednesday, December 2, 2009

VIDEO YA LADY JAY DEE TEJA IME LEACK


Hii ni habari kutoka kwa mwanadada Lady JD "Video ya Teja ime LEAK wala sija Release, nashangaa ni nani ameamua kufanya hivyo? Yote kheri tutaendelea tu kukomaa mpaka tuone mwisho"

Tuesday, December 1, 2009

BARUA NZITO KUTOKA KWA PRODUCER BANO KWENDA STUDIO ZA TONGWE RECORDS


Habarini ndugu zangu watanzania?

I hope kila mtu yu salama.Nimeamua kuchukua fursa hii kuongea na umma juu ya roumuz zinazo nikabili mimi.Ningependa watu waajue kuwa J-RYDA was a close friend of mine hata J-MURDA naye pia.I wonder why wameamua kunifanyia hivyo by this hour?TONGWE was facing a problem by the time producer wao DUKE anaondoka studio so they needed a producer & J-MURDA was a brother of my school mate so ikawa rahisi kunipata mimi.I started producing the songs tongwe kuanzia mwezi march mpaka july.Kukaanza kutokea matatizo baina yangu mimi na the owner coz alishindwa kunilipa pesa za matangazo ambazo zilikuwa zimebaki,tuligombana sana then nkaona ngoja nirudi nyumbani.Nikawa naenda studio when im needed nkawa sijiendei tu.By august nkaanza kumpeleka J-RYDA studio with our fellow producer named carson-g.By 26 of august me nkasafiri kuja kusoma which means me na j-ryda kama kukaa tongwe studio me na yeye its jus only 3 weeks ambazo in real sense hakuna production isiyozidi nyimbo 3 hata kama mtu una usongo gani u cant produce more than 3 songs pre 3 weeks.

Yeye kuclaim me nimeondoka nanyimbo zake its meaningless coz they know dat me nlikuwa nimeproduce nyimbo ngapi before mimi kuondoka tho by the time me naondoka ni nyimbo moja tu ''watoto wa mjini'' ya jos mtambo & chidi benz ndio iliyokuwa imetoka.Alaf ever since i started my music career sijawahi kutengeneza pesa yeyote ile kutoka kwenye music,so i hope u pipo can feel the feeling ambayo i am going through rightnow.

Tukiwa studio kuna vitu vingi sana vinatokea kwa mfano;u can make the whole song alaf ukamsikilizisha mwenzio akupe comments zake then maybe anakwambia the bass haijakaa vizuri then unamwambia put it the way u want,akishafanya then off u go.Sasa beat za style hii zipo nyingi sana ambazo me na RYDA tumefanya ever since kitambo till 2day.Angesema hizo ndio zake kidogo ningemuelewa but he did not do that.

Talking about goodboi,nimerudi ya cyrill and further songs kuwa they are not my art haya aseme but in heart he knows.Nikianza kugombania nyimbo ambazo they are about to fade out ni ujinga!!! kama anaclaim ameproduce si kuna nyimbo mpya ambazo yeye ameproduce do they vary na hizo ambazo nimeproduce?!!!!

Furthermore,alikuwa wapi kusema hivyo muda wote nyimbo zinatoka naenda kwenye interviews sometimes i even forget na ye huwa ananikumbusha dat yo boi u got these interviews and all dat.Siku ambayo me naondoka nakumbuka niliwatumia texts yeye na our other fellow CARSON -G dat i did not take them to the spot ambayo nlitaka tufike so they shud fight for that coz atleast mimi nimeweza kuwafungulia njia so it wili be easy for them to reach up.

3 weeks kabla ya leo ilininbox na kuanza kuniambia dat i think its time for him to go on alone with the music career so its like he duznt need me anymore.Ila kama ni goodtymes tule pamoja kama kawaida.The way nilivyomuelewa mimi its like alikuwa ananidump, nkamwambia poa.We were talking about so many things even future projects and all dat so dat means kulikuwa hamna tatizo lolote.

J`mosi ambayo wamefanya interview usiku wake we were on facebook chatin as if he did not do anything to harm me.Sunday nkaanza kupokea simu kutoka kwa watu tofauti wakiniambia about this,nkasema ngoja niulize imekuwaje.Nkampigia Cyrill and he told me the same thing,nkaongea na dozen ye ndio akaniambia dat they did the interview na wewe so dats why i decided to txt you.Niliongea na nick wa pili na watu kadhaa kila mtu akawa anashangaa.

Nway,

They shud come up with a new plan ya kuinyanyua studio but not kuwa mislead my pipo.And kuhusu nyimbo kudistribute online!
naomba wanitajie hizo webs ili nizidistribute kweli sasa without a doubt coz itakuwa haileti maana kama nikizificha tena.And i promise them kila baada ya siku 3 ntakuwa nazitoa kweli.Wanitajie web moja tu nifanye kazi yangu.
Kukaa kunipakazia vitu vya ajab ni si busara njema kwani ni kunidhalilisha na si kuniaibisha.Kama wanataka kunyanyua studio kwa style ya roumuz studio itakufa mapema sana.Alaf J-MURDA anasahau kwamba nilikuwa shule nkawa naproduce nilipohitajika shule nkaacha kuproduce which means hata RYDA nae atakuwa studio and then ataondoka kama nilivyofanya mimi.Wanatakiwa wafurahi kwamba i paved the way for them to succeed not to knock me down.

Sitatoa nyimbo hata moja ambayo nimefanya kuanzia 2007-09 so nawaruhusu wazitumie hizo nyimbo ambazo niliziacha zije kutoka baadae,wafute zile tags zangu zote waweke zao its okay i wont mind.I will just start a new page of my music career with not more than 50 songs to say goodbye to ma fans,my music career is over according to me.Sitaproduce anymore song zaidi ya hizo and i will just want to prove them wrong.NITAFANYA HIVI SI KWA KUTENGENEZA BATTLE WITH THEM BALI KWA KUWAFANYA WATENGENEZE VITU VIZURI KAMA VYANGU,KWANI WALIVIONA NI VIZURI NDIO MAANA WANAVIGOMBANIA.

Alaf i got a good msg for them, wasikilize lyrics zangu za nyimbo ya ''ON FIRE'' watajihisi niliwataja wao and its true coz i was prepared for this to happen 1 year ago.So i am forever prepared they shud get a new plan.Money its juss the other side of life so wasichanganyikiwe sana 200,000 kuna millions and billions watu wanashika na still they act cool.

Nawatakia kila la kheri katika maisha yao ya kimuziki.And thanks pia kwa watu wote watakao kuwa bega kwa bega na mimi katika hili.

Thanks to u once again,

Yours,
Bano Stylez Dha General

TUSIJISAHAU JAMANI


Siku ya Ukimwi Duniani inakumbukwa kila tarehe kwanza Desemba. Hii ni siku maalum ya kupanua ufahamu kuhusu maafa yanayoletwa na ugonjwa wa Ukimwi. Desemba kwanza ilichaguliwa kuwa ni siku ya Ukimwi kutokana na tarehe hiyo kuwa ndio siku ambayo kirusi cha Ukimwi kilitambulika rasmi mwaka 1981. Toka mwaka 1981 watu zaidi ya milioni 25 wameshafariki kutokana na Ukimwi.

Siku hii ilichaguliwa rasmi mwaka 1988 wakati wa Mkutano wa Dunia wa Mawaziri wa Afya Kuhusu Mpango wa Kuzuia Ukimwi. Kuanzia hapo siku hii imekuwa ikikumbukwa rasmi na serikali, mashirika yasiyo ya kiserikali, na wanaharakati.

Toka mwaka 1988 hadi 2004, Siku ya Ukimwi Duniani ilikuwa ikiratibiwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Masuala ya Ukimwi (UNAIDS). Mwaka 2005 UNAIDS ililipa shirika lisilo la kiserikali la Kampeni ya Ukimwi Duniani (the World AIDS Campaign)wajibu wa kuratibu siku hii.

Kila mwaka siku hii hukumbukwa kwa ujumbe maalum. Ujumbe wa mwaka 2005 ni Zuia Ukimwi: Timiza Ahadi. Ujumbe huu utatumika hadi mwaka 2010.

Monday, November 30, 2009

MREFU NA MFUPI KULIKO WOTE DUNIANI


mtu mrefu kuliko wooote duniani akisalimiana na mtu mfupi kuliko wote


“Bao Xishun,ameandikwa katika kitabu cha record za dunia kama ndio mtu mrefu kuliko wote wanaoishi duniani akiwa na 7ft na inchi 8.pichani yuko na mkewe xia shujuan

Friday, November 27, 2009

BUSTA RHYMES LIVE NA MZUKA WAKE FIESTA 1 LOVE 2009


Find more videos like this on G5 world

Wednesday, November 25, 2009

MDAU WA ZE BLOG


Mdau wa ze blog hii, Allen Sobo anawapa anawapa hi! wooote

Tuesday, November 24, 2009

WASHINDI WA FIESTA ONE LOVE KIMYA KIMYA



hawa ni baadhi ya wahindi wa fiesta one love kimya kimya ambao walijishindia zawadi kibao kutoka zain, nokia na serengeti ikiwa ni pamoja na pesa taslim kutoka Clouds Fm

HAPPY BIRTHDAY DINA MARIOS



bonge la keki unabishaaaaaaaaaaaa

Friday, November 20, 2009

FIESTA ONE LOVE 2009 REHESAL.....


stage la fiesta pne love 2009 linayoonekana kabla halijamaliza kutengenezwa jana usiku wasanii wote walikuwepo kwaajili ya rehesal

qj aliniambia sio kuimba tu hata nguzo mojawapo ya hiphop anaiweza pia



kutoka kushoto ni b12, fe'e na quick racka

mwanadafada baby madaha na maunda wakisubiri zam yao

Wednesday, November 18, 2009

MORRACA AJITOA RACKAS


the sexsiest men muite morraca
muasisi na muanzilishi wa kundi la rackas lenye vichwa vikali ndani nawazungumzia quick racka, chief racka na dowracka amejitoa katika kundi hilo kwasababu ambazo yeye mwenyewe hakuzisema.morraca amesema amejitoa kundini lakini sababu atazifafanua zaidi sio muda mrefu.utapata updates mara tu taarifa zitakaponifikia

kundi zima la rackars

Tuesday, November 17, 2009

MTOTO HUYU PIA HUTOKWA MACHOZI YA DAMU


hii sasa inaanza kama kushangaza baada ya kufikia watu watatu kuwa na tatizo hili la kutokwa na mchozi ya damu badala ya machozi ya kawaida (maji).mtoto huyu anaitwa TWINKLE ambae kwa hivi sasa anapata miaka mwili sasa.mtoto huyu hutokwa na damu utosini, kiganjani, miguuni, na machoni na sehemu zinginezo.

ATOKWA NA MACHOZ YA DAMU KILA ATOAPO MACHOZI



MWANAMKE nchini India, Rashida Khatoon, amekuwa gumzo nchini humo kutokana na hali yake ya kutoa machozi ya damu kila anapolia.Rashida amewashangaza hata madaktari kwa hali yake hiyo ya kutiririka machozi ya damu kila anapolia.
Kwa siku mwanamke huyo humwaga chozi la damu mara kadhaa."Sisikii maumivu yoyote, badala ya machozi ya kawaida, damu zinapotitirika ni kitu cha kushangaza" alisema mwanamke huyo.

Viongozi wa dini wa India wanadai kwamba mwanamke huyo ni miujiza toka Mungu.

Monday, November 16, 2009

JOSE MTAMBO NDANI YA ONE LOVE MWANZA


Find more videos like this on G5 world

KAAAAAAA HUMOOOOOO

BONGO FLEVA FIESTA FREESTYLE MC SHUJAA ILIKISANUA MBAYA MJENGONI


mzuka ukipanda habari ndio hiii mtu mzima ncha kali mc of that day

mr climax in the house

The king himself Lusajo jackson ambae ndie aliekuwa mshindi wa Bongo fleva frestyle mc shujaa mwaka 2008 akitema madini kumbattle mkali wa freestyle Mr climax na kumtupa kuleee

An upcoming artist na mmoja kati ya watashambulia jukwaa la fiesta mwaka 2009 muite Bekha Tittle akiperfom ngoma yake (mwendo wa maringo)

Director mwenyewe nilikuwepo kumake sure kila kitu kinaenda sawa. kulia ni producer Lamar na kushoto ni Young D

Mteganda akishow love na Baghdaa baada ya kumtupa kule Baghdad na kuingia fainali

Camera man kutoka clouds tv (Kabezi) akichukuwa matukio kwa ajili ya clouds tv

Majaji waliokuwa wakiendesha show nzima kuwatafuta wakali wawili watakaowakilisha kwenye fainali ndani ya fiesta one love 2009. kushoto ni Saigon pamoja na dj steve b Dj skills

Baghdad kulia akiwa na X dizzo wakisubiri time yao ya kubattle

Moo myama akichanana na Sticky yicky

Adam mchovu a.k.a Brother from another mother akiwa live na radio ya watu na huyo mwingine ni Dj aron

Hawa ndio wawakilishi wa camp za kula raha na burudani pamoja na energy ya kushangilia waliojichukulia tickets 20 kila camp pamoja na zawadi kibao za fiesta one love. camp hizo ni Dar mob kutoka makumbusho, Wabishi camp kutoka kiwalani, Wadon town kutoka kigogo mbuyuni, Mishen not complete kutoka kigogo na The swaga brothers kutoka kigogo

G NAKO NDANI YA CHIZIKA BASH IJUMAA



g nako akiwa na bou nako

mtu mzima niki wa pili
Gnako na Nick wa pili walikuwa ndani ya chizika bash ijumaa ya tarehe 13,waliwapa wa2 mpango mzima yaani show nzito licha ya tanesco kufanya vioja vyao mara kadhaa machizi wakiwa jukwaani hivo kupelekea watu kukatishiwa stim walizolipia...mzuka ulirudi majenereta yalipoamshwa na kazi ikaendelea kama kawa!...kwa waliohudhuria,ukweli ni kwamba hiphop aint dead asee!..